Polisi Afumaniwa Akichepuka Mwezi Mmoja tu baada ya Kuoa


Polisi

Afisa wa polisi nchini Kenya aliyefunga ndoa Desemba mwaka jana, amefumaniwa chumbani akiwa na mke wa mtu, katika nyumba moja mtaa wa Eastlands jijini Nairobi.

Mwanamume huyo aliyemfumania Afisa wa Polisi, imeelezwa kwamba alikuwa amesafiri kwenda kijijini na aliporudi nyumbani akamkuta mkewe akimsaliti.

Baada ya majibizano ya muda mfupi, mwanaume ambaye amefahamika kwa jina la Ali Abdul Majid, alihisi kutishiwa maisha na kuamua kupiga ripoti katika Kituo cha Polisi cha Dondora.

Maafisa wenzake mtuhumiwa waliotoa michango katika sherehe yake ya harusi walishangazwa kabisa na kisa hicho.

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post